karibu

kwa habari moto moto

Monday, November 30, 2015

sheikhe ponda aonekana hana hatia

 Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoa wa morogoro  imemuachia huru Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Issa Ponda aliyekuwa akituhumiwa kwa makosa ya uchochezi na kesi ya jinai baada ya mahakama kutoridhishwa na ushahidi wa upande wa mashtaka na hivyo kuonekana hana hatia

Makosa yaliyokuwa yakimkabili ni mawili ambayo ni kushawishi watu kutenda kosa, pamoja na kutoa matamshi yanayoumiza imani ya dini nyingine.

Hakimu wa kesi hiyo Mary Moyo amesema ushahidi uliotolewa na upande wa mashitaka haukujitosheleza hivyo mahakama hiyo imemwachia huru na rufaa iko wazi endapo upande wa mashitaka hautaridhika na hukumu hiyo.
Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu
                                     picha ya sheikhe ponda issa ponda

jaji alie kuwa anasimamia kesi hiyo  amemshauri sheikhe ponda kufungua kesi ya bakwatwa na kampuni agritanza limited aliyo uziwa eneo la waislam lililopo chang`ombe jiji dar es salaam na ame mshauri aisende kwa namna nyingine bali atumie njia ya mahakama,, pia imemuachia kwa kipindi cha miezi 12 kwa shart la kutofanya kosa lolote

source;mwanachi
source:east africa

No comments:

Post a Comment