kwanini na thubutu kusema hayo labda turudi nyuma baada ya kuchaguliwa kuiongoza nchii hii kwa awamu ya tano dk John pombe magufuli kitu ambacho watu walitegemea kuteua waziri mkuu ambae wote walijua Mh Herison mwakyembe hili halina ubishi ndani yake
kila mtu alikuwa na matumaini makubwa kuwa mwakyembe kutokana na kasi yake wangeendana na magufuli
kwa mshangao na hali isiyo tarajiwa magufuli amemteua mh Kassim Majaliwa kuwa waziri mkuu wa jamhuri ya muungano wa Tanzania, sio kwamba majaliwa hakuwa ana fahamika la hasha majaliwa alikuwa anafahamika ila wengi hawakudhani atakuwa waziri mkuu hata kwa 1% kasi yake na utawala wake baada ya kupewa nafasi hiyo watu tunaiona sasa
turejee katika mada kuu usiku wa kuamkia jumapili baraza kuu la chadema lilikuwa na kikao kizito ambacho ilikuwa ina mtafuta mtu ambae ata vaa viatu vya dk wilbroad slaa ambae aliachia ngazi kipindi cha uchaguzi mkuu 2015 baada ya kutofautiana na washirika wenzake mara baada ya kumkaribisha Edward lowasa na kumsimamisha kuwa mgombea wa chadema na ukawa
Mbowe naye ikampata ya magufuli alikuwa na changa moto hiyo ya kumchagua katibu mkuu naaminimajina yalikuwa mengi na labda watu walikuwa na hisia tofauti na huyu akie chaguliwa, nilipata kusikia watu wengine wakisema mh LISSU wengine Salim mwalim lakini yote kapuni
bila ya uoga mh vicent masinji amechaguliwa kuwa katibu mkuu wa chama hiko ambae nae hakuwa anatajwa na wengi na watu hawakutarajia kama masinji atakuwa katibu mkuu
hii ina msaidia mbowe kutopata maswali mengi kutoka kwa waandishi mbali mbali kutokana na ushujaa huu wa kuchagua mtu asiye fahamika baadae anafanya kazi ambayo wengi inakuwa kama mshangao kama ilivyo kwa majaliwa

hii sasa inakomesha dhana ya mapendekezo ya watu pasipo ufuatiliaji kuwa nani anafaa na anaweza endesha sisa katika mlengo wa maendeleo
binafsi mimi mtoa makala simfaham sana lakini hii ya kutushtukiza ina leta tija kuliko hii tulie zoea. sijajua kama ndio sisa inakua au vipi jibu unalo wewe .
kikubwa na heri tuombe amani ya nchi yetu ili isiingie machafuko tuweze kuona mengi ambayo hatukuweza kuyaona katika vipindi vilivyo pita.