Baada ya kufungua kesi ya kubatilisha uchaguzi wa ubunge uliofanyika 30.10. 2010 kutokana na masharti ya uchaguzi huo kuvunjwa na msimamizi wa kuhesabu kura kutenga ukumbi mwingine wa T.C.C kuhesabu kura hizo badala ya ukumbi uliopangwa wa manispaa ,
Hayo ni maelezo ya mfungua kesi hiyo ndugu ULEDI HASSANI ABDALLAH aliye gombea ubunge kupitia chama cha C.U.F wakati akitoa maelezo kwa jaji bwana SULEIMANI SAIDI KIHIYO kuomba mahakama hiyo ibatilishe ushindi wa HASNIN MOHAMEDI MURIJI mgombea wa ccm kutokana na
kutotendewa haki wakati wa kuhesabu na kutangaza matokeo
Aidha katika majumuisho hayo pia wakili wa upande wa mdaiwa JOSEPH KADAYO na FARAJI MCHIMBI wao wamepinga maelezo hayo hayana ushahidi wa kutosha kutokana na ushahidi huo kutolewa kwa mdomo bila ya nyaraka yeyote
Aidha baada ya kuhitimisha majumuisho hayo jaji wa kesi hiyo bwana SULEIMANI SAIDI KIHIYO ameahirisha kesi hiyo hadi octoba 18 hukumu itakapo tolewa
No comments:
Post a Comment